Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Waziri Gwajima akizungumza na wagonjwa hao hii leo.

Na Veronica Mrema – Dar es Salaam

Mkazi wa Dar es Salaam, Mbwana Said, ametamani kuchana kipande cha shati lake na kumpatia Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Doroth Gwajima, akidai kwamba anavutiwa na utendaji kazi wake.

Said ni miongoni mwa wagonjwa waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala hii leo ambako Waziri Gwajima alifanya ziara kukagua namna wanavyotoa huduma kwa wananchi.

“Ingewezekana mama (Dk. Gwajima), ningeomba leo nichane kipande cha shati langu, uende nacho kiwe ukumbusho kwako, hongera kwa kufanya kazi nzuri,” amesema Said mbele ya hadhara iliyokuwa imeambatana na Waziri huyo kila mmoja akijikuta anaangua kicheko.

Awali, Said na wenzake, Leila Mussa na Salma Juma walimueleza Waziri huyo kwamba wanaishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za afya, hata hivyo kilio kilichopo sasa ni kuhusu gharama za matibabu.

Waziri Gwajima aliwauliza iwapo wanafahamu kuhusu suala la kukata bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa (CHF), Said alisema yeye amekwisha kukata, lakini Leila na Salma walishangazwa na jambo hilo kwamba hawalifahamu.

“Binafsi sijui, kama kuna hiyo bima naomba nieleweshwe ili nikate, maana ninaugua kisukari, gharama za dawa ni kubwa kuna wakati nashindwa kumudu na sisi wagonjwa wa kisukari wakati mwingine huwa tunapata vidonda,” amemueleza Waziri Gwajima.

Kutokana na hilo, Waziri Gwajima ametoa maelekezo kwa waganga wakuu wa mikoa, wilaya na timu wanazoziongoza za afya na ustawi wa jamii, kuhakikisha zinajipanga kwenda ngazi ya chini ya jamii ili kutoa elimu kwa wananchi.

“Inanishangaza, wananchi wanataka kujiunga, hawana taarifa, mnafanya nini?... ofisa ustawi wa jamii, anastawisha nini?..,” amehoji.

Waziri huyo amesisitiza “Serikali inaelekea katika bima moja, lazima wananchi waelimishwe na wakate bima ya afya.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement