Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema – Dar es Salaam

Daktari mmoja wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, yupo matatani kwa madai ya kuchukua rushwa ya kiasi cha Sh. 700,000 kutoka kwa mgonjwa mmoja (majina yamehifadhiwa) na kumfanyia upasuaji hospitalini hapo, pasipo uongozi kujua.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Doroth Gwajima (aliyevaa kitenge pichani) ameweka wazi hilo leo alipotembelea hospitali hiyo kukagua hali ya utoaji wa huduma.

Amemuelekeza Mganga Mfawidhi wa Amana, Dk. Amani Malima kuhakikisha daktari huyo anafuatilia suala hilo na daktari huyo anachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo ikiwamo kufikishwa mbele ya baraza la maadili.

Dk. Gwajima amesema anazo taarifa zote muhimu kuhusu daktari huyo ambazo amezipata kutoka kwa mgonjwa aliyemuhudumia.

Waziri huyo amesema tukio hilo limefanyika Novemba 30, mwaka huu hospitalini hapo na mgonjwa huyo amemueleza hayo na kumpatia ‘chart’ (mtiririko wa mawasiliano) kati yake na daktari huyo ambazo zilifanyika kwa njia ya mtandao wa ‘watsup’.

“Nilitoa mawasiliano yangu, wananchi wananifikishia malalamiko mengi kuhusu Amana, huyo daktari akijua kwamba amefanya kosa, mgonjwa alilazimika kwenda kupanga chumba nje ya hospitali, akatafuta muuguzi mwenyewe ambaye alimuhudumia kidonda chake hadi kilipofunga, alimkodia hadi teksi ya kumpeleka huko aendako.

“Kidonda kilipofunga, mgonjwa alirudi kudai risiti lakini hakupatiwa hadi leo, jinsi walivyowasiliana kwa njia ya watsup, amenitumia kila kitu, huyu lazima apatikane, andike maelezo na achukuliwe hatua hadi baraza la maadili,” ameagiza.

Waziri Gwajima amesema wakati umefika kwa watumishi kubadilika, kuwajibika na kufanya kazi zao kwa weledi na kuzingatia miiko na maadili yao.

“Nimetoa muda wa siku 90 kuanzia sasa, kila kiongozi katika kila eneo alilopo kuhakikisha anajua wajibu wake, zitakapotimia nitajua cha kufanya, ‘tutawachekecha’,” amesisitiza.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement