Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema – Dodoma

Walimu wakuu wa shule zote nchini wameagizwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kukagua miundombinu ya umeme mashuleni, ili kuepusha matukio ya moto ambayo hivi karibuni yameripotiwa maeneo mbalimbali nchini.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako ametoa agizo hilo leo alipokuwa akifunga Mkutano Mkuu wa 15 wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) uliofanyika jijini hapa kwa siku tatu (Desemba 20 hadi 22, mwaka huu).

“Hivi karibuni yameripotiwa matukio ya shule kuungua moto, imarisheni ulinzi na usalama wa shule, shirikianeni na TANESCO), kukagua miundombinu ya shule kama ipo salama au la,” ameagiza.

Waziri Ndalichako aliwaagiza walimu wakuu hao kuhakikisha pia wanasimamia nidhamu za walimu wanaowasimamia shuleni ikiwamo katika suala la mavazi, wavae yenye staha.

“Nyie nikiwaangalia mmependeza kweli kweli, nendeni mkawasimamie na walimu wenu vizuri, wavae mavazi yenye staha na wale wasiozingatia wachukuliwe hatua za kinidhamu, vivyo hivyo kwa wanafunzi,” ameagiza.

Naye, Naibu Waziri kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, David Silinde, amesema tayari mwongozo wa usimamizi wa nidhamu kwa walimu umeshaandaliwa, utasambazwa wakati wowote kuanzia sasa kwa ajili ya utekezaji.

“Naamini mwongozo huu utakapotoka, utasaidia kufanikisha usimamizi wa nidhamu kwa walimu, kwa sababu tumeshawafukuza na hata kuwashusha vyeo lakini bado kuna changamoto, mwongozo tunaotarajia kuutoa utasaidia kukabili changamoto hii,” amesema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement