Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Walimu wakuu shule za sekondari wakiwa kwenye mkutano mkuu wa 15 wa TAHOSSA.

Na Veronica Mrema – Dodoma

Serikali imejipanga kufanya msako wa uhakiki wa vibali vya walimu wa kigeni nchi nzima ikisisitiza waajiri (wamiliki) wa shule hasa za binafsi kuzingatia kanuni na sheria za nchi katika kuajiri.

Yameelezwa hayo leo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, alipokuwa akifunga Mkutano Mkuu wa 15 wa Wakuu wa Shule za Sekondari uliofanyika jijini hapa kwa siku tatu (Desemba 20 hadi 22, mwaka huu).

Waziri Ndalichako amesisitiza katika jambo hilo Serikali haina mzaha na kwamba tayari ina taarifa muhimu watakazoanza nazo wakati wa msako huo.

“Nawasihi waajiri (wamiliki) hasa wa shule binafsi kuzingatia miongozo ya Serikali katika kuajiri, tunazo taarifa za awali kwa sababu tumefanya tathmini baadhi yenu mnakiuka.

“Shule binafsi baadhi zinakiuka, Sheria za nchi kwa kuchukua walimu nje ya nchi na wanajua wazi kufanya kazi nchini bila kibali ni makosa,” amesema.

Ameongeza “Tunajua hivyo vichaka, anzeni kuchoma moto vichaka vyenu wenyewe, tunakuja kufanya tathmini ya kina, nawasihi walimu wakuu wa shule za binafsi za sekondari, anzeni kutoa taarifa kwa wamiliki wenu, tunakuja.

“Msipotoa taarifa mapema, kwa sababu mnajua… tukija huko kukagua mtaipata,” amesisitiza.

Pamoja na hilo, Prof. Ndalichako ameagiza mazingira ya shule zote nchini kuwekwa katika hali ya usafi kwani katika baadhi ya shule alizotembelea amekuta ni machafu huku madarasa yakiwa yamejaa buibui.

Awali, Naibu Waziri kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), anayeshughulikia masuala ya Elimu, David Silinde, ameagiza wakuu wa shule na wakurugenzi wote nchini kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa madarasa kufikia Februari 28, mwaka huu.

“Ili wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza, waanze masomo yao,” amesisitiza.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement