Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema – Dar es Salaam

Asilimia 80 ya wananchi wanaojitokeza kuchangia damu ndani au nje {kwenye kampeni maalum za uchangiaji damu zinazofanywa na..} Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala {RRH}, hukimbia/hutelekeza majibu yao.

Yameelezwa hayo na Mtaalamu wa Kitengo cha Maabara Huduma za Damu Mwananyamala RRH, Loveness Sunda katika mahojiano maalum na MATUKIO NA MAISHA BLOG yaliyofanyika wakati wa maonesho ya hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru.

Amesema Mwananyamala RRH ni miongoni mwa vituo vya uchangiaji na ukusanyaji damu salama Kanda ya Mashariki, Wilaya ya Kinondoni, kiasi cha damu kinachokusanywa na kituo hicho husaidia pia kuokoa maisha ya wagonjwa kwenye hospitali nyinginezo.

Ametaja baadhi ya hospitali wanazozihudumia pamoja na Mwananyamala yenyewe ni Kairuki, Saifee, TMJ, Kinondoni Hospitali, Kituo cha Afya Sisa na vituo vingine mbalimbali.

“Wengi {wanaojitokeza kuchangia damu} wanaogopa kuja kupokea majibu yao, wanayakimbia, tunadhani wengi huhofia kuja kuchukua pale wanapofikiri kwamba endapo si mazuri itakuwaje,” amesema.

Ameongeza "Wakija kwa mara nyingi kuchangia damu kwa sababu anakuwa na ile namba yake kwenye 'data base' yetu tunafuatilia 'status' yake kama majibu yake ni mazuri tunaendelea naye kama si mazuri tunamuelekeza nini cha kufanya.

Loveness amesema pamoja na hayo, kiasi kingi cha damu huchangwa na kundi la wanafunzi ambao wengi wao hufuatwa ma-shuleni/vyuoni na kwamba kwa asilimia 90 damu zao huwa salama.

“Yaani tukienda kukusanya damu kutoka kwa wanafunzi tuna uhakika kwamba kama tumekusanya chupa 100 basi chupa zipatazo 90 huwa ni salama kwa matumizi/kuokoa maisha,” amedokeza.

Amesema kiasi cha damu kinachohitajika kutosheleza mahitaji ya hospitali hiyo na nyinginezo ambazo wanazipatia ni wastani wa chupa 500 hadi 550 kwa mwezi hata hivyo kiasi kinachopatikana ni chupa 300 hadi 350 pekee.

“Idadi hii ni sawa na kiwango cha asilimia 60 tu ya mahitaji yetu, hatujawahi kufikia kiwango cha asilimia 100,” amebainisha Ofisa huyo kutoka Kitengo cha Maabara, Huduma za Damu Mwananyamala RRH.

Ametoa rai “Hivyo bado tunaendelea kuhimiza jamii, kujitokeza kuchangia damu kwani mahitaji ni makubwa hasa kwa kundi la wajawazito wanaokuja kujifungua, majeruhi wa ajali mbalimbali hasa za barabarani na wagonjwa wengine wanaolazwa hospitalini.

Hospitali hiyo iliyoanzishwa mnamo mwaka 1973 kama kliniki hususan ya masuala ya uzazi ilifanya maonesho hayo {Desemba 6 – 8, 2021} ili kuwaonesha wananchi huduma zake wanazozitekeleza katika idara zipatazo 15 walizonazo.

Wananchi walipata fursa ya kuchunguza afya zao na kupewa ushauri bila malipo huku wengine wakifika kupata chanjo za UVIKO – 19 kwenye maonesho hayo.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu inasema ‘Miaka 60 ya Uhuru Tanzania Imara, Kazi Iendelee.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement