Afrika Kusini
Mtanzania Ahmadi Mbwana Chonde (50) amekamatwa na Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya cha Jimbo la Gauteng Nchi Afrika ya kusini akiwa na Dawa za kulevya aina ya heroin kilo mbili.
Taarifa iliyotolewa usiku huu na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya {DCEA} kwa vyombo vya habari imeeleza Chonde alikamatwa nchini humo Desemba 20, 2022 katika uwanja wa ndege wa jijini Cape town.
DCEA imeeleza, Chonde alikamatwa akiwa hati ya kusafilia yenye namba TAE145658 akisafilisha dawa za kulevya akitokea mji wa Capetown nchini Afrika ya Kusini kuelekea nchini India katika miji ya Kochi na Chennai kupitia Doha.
Katika taarifa hiyo, imeelezwa Mtanzania huyo alikuwa ameficha dawa hizo za kulevya ndani ya sanduku lake alilokuwa akisafiri nalo.
Chapisha Maoni