Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Na Veronica Mrema

Upatikanaji duni wa huduma rafiki za masuala ya afya ya uzazi bado ni ‘mwiba’ kwa kundi la vijana, nchini Tanzania.

Kukosekana elimu, stadi na miongozo sahihi ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana kunatajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa vijana kujiingiza katika tabia hatarishi ikiwemo ngono zisizo salama.

Athari za vitendo hivyo ni pamoja na mimba zisizotarajiwa, magonjwa ya ngono  na matumizi holela ya dawa za kuharibu mimba.

Kuna ongezeko la wasichana wanaopata ujauzito katika umri wa miaka 15 hadi 19 ambapo kipindi cha mwaka 2010 idadi ilikuwa 23% lakini imefikia 27% mwaka 2015/16.

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa ripoti za TDHS zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

Akizungumza,  Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao unaojihusisha na masuala ya Ukimwi na Afya Ukanda wa Afrika Mashariki {EANNASO} Onesmus Kalama amesema..,

“Upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi kwa vijana bado haujawa rafiki kwao, wengi wanaogopa kwenda kwa sababu ni sehemu mchanganyiko.

“Kijana anaangalia je nikikutana na shangazi yangu itakuwaje?,” amesema na kuongeza

“Ndiyo maana unakuta wengi wanakimbilia famasi wanajinunulia bila kufuata maelekezo kwa daktari ambayo ni athari kubwa.

Amesema kwa sababu dawa nyingi wanazojinunulia hupaswa kutolewa kwa mwongozo wa daktari lakini wao huambizana wenyewe na marafiki kwenda kununua.

“Hawajui dawa zile wanameza zitakuwa na athari gani hapo mbele,” amesisitiza.

Tanzania bado inatajwa miongoni mwa nchi zenye viwango vya juu vya ndoa za utotoni duniani, ripoti ya TDHS ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu 2015/16 imesisitiza.

Kulingana na ripoti hiyo, miongoni mwa wasichana wenye umri wa miaka 20 hadi 24 ambapo 5.2% waliolewa wakiwa na miaka 15 huku 30.5% wakiwa na umri wa miaka 18.

Lilian Lema ambaye ni mtengeneza maudhui mtandaoni yanayoangazia afya ya uzazi hususan kwa kundi la vijana amesema elimu kuhusu afya ya uzazi ni muhimu kwa kundi la vijana.

“Kwani inasaidia vijana kujikinga na magonjwa ya ngono, mimba za utotoni, wanawake wazazi ni  namna gani ya kujikinga kipindi cha uzazi mpaka wanapojifungua na hata masuala ya hedhi salama.

Naye, Mkurugenzi wa Binti Salha Foundation Salha Haziz amesema “{Tanzania} tupo ‘level’ ambayo tunapokea mabadiliko kuanzia ngazi ya juu Serikalini hadi chini {katika eneo la afya ya uzazi}.

Ameongeza “Elimu inaendelea kutolewa na kufanya uchechemuzi kwenye kuboresha Sera zetu kuweka fedha za kutosha kwenye eneo hili.

“Pia vijana kupata elimu na huduma rafiki ili kuweza kujitambua na kufanya maamuzi sahihi, lakini bado kuna changamoto huduma rafiki na zisizo na unyanyapaa.

“Bado vijana wanakumbana na unyanyapaa kiasi kwamba wanaacha kufuata huduma rafiki kwenye vituo vya afya ambako Serikali inawekeza fedha nyingi.

“Matokeo yake wanafuata hizo huduma sehemu ambazo si sahihi au wanakwenda kupata huduma kwa watu wasio sahihi matokeo yake wanafanya vitu ambavyo wengi wao vinaharibu maisha yao.

Amesema kuna mimba za utotoni.., zisizopangwa, kuna wanaopoteza uhai kwa kutoa mimba kwa njia zisizo salama, au wanapata virusi vya ukimwi na ukimwi pale wanapotumia njia zisizo salama.

Kalama ameshauri ni muhimu kuhakikisha upatikanaji wa huduma rafiki za uzazi kwa vijana zinakuwapo ili wawe na uwezo wa kwenda katika vituo vya kutolea huduma za afya na si kwengineko.

1 Maoni

Chapisha Maoni

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement