Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Na Veronica Mrema

Kaya zaidi ya 98% zilizopitiwa na mradi wa bomba la mafuta ghafi [East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP] tayari wamefikiwa na kulipwa fedha kwa mujibu wa Sheria ili kupisha mradi huo, Tanzania.

Ujenzi wa bomba hilo unachukua kiasi cha Km 1,443 kutoka Kabaale Uganda hadi Chongoleani Tanga, ambapo mafuta hayo yatapakiwa kwenye meli tayari kusafirishwa nchi mbalimbali.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano EACOP kwa upande wa Tanzania Catherine Mbatia amesema bomba hilo litapita katika mikoa minane Tanzania.

Amesema tayari wamegawa nyumba 339 kwa waathirika ambao walichukuliwa makazi yao kwa kupitiwa na mradi huo.

Ameongeza “Mwezi Uliopita tumegawa nyumba ya mwisho ya mnufaika, tulikuwa na wa aina mbili kuna waliochukua ardhi tupu na kuna waliochukuliwa makazi yao [nyumba] walikuwa 339.

“… na mwezi ulioisha tumempa mwathirika wa nyumba 339 Tanga na wale waliochukuliwa ardhi zao namaanisha mashamba na waliopewa ‘composition’ kwa njia ya fedha karibu wote wameshalipwa.

“Wale waliopatikana na wale ambao hawajapatikana fedha zao zipo, tuna anuwani na majina yao, tumeshatangaza kupitia vyombo mbalimbali vya habari kwa kutumia redio za jamii na Taifa.

Amesisitiza “Tumefanikiwa kupata wengi, tumebaki na wachache na hao fedha zao zimehifadhiwa, wakati wowote hata kama mradi utaisha wakija na vielelezo sahihi watalipwa.

“Mradi unaendelea tumeshuhudia mwanzoni mwa Desemba hii tumepokea mabomba, yanayokwenda kuwekwa Km. 100.

“Tunafahamu kwa Tanzania mradi huu una Km. 1443 ni mwanzo mzuri tumeanza kupokea mabomba yatakayowekwa Km. 100.

Amesema hii inaonesha kwamba ule mradi ambao Watanzania wamekuwa wakiusikia siku zote sasa unakwenda kutekelezeka.

“Walikuwa na hamu ya kuuona unatekelezeka kwa kupokea mabomba hayo inaonesha sasa kazi imeanza na mradi wetu upon a Watanzania tutaendelea kunufaika zaidi na zaidi,” amesisitiza.

Kitovu cha mradi huo ni katika Ziwa Albert huko Uganda ambapo 80% litapita upande wa Tanzania kwa kiwango cha Km. 1,443 na Uganda ikiwa na Km. 296.

Kampuni ya Total Energy inamiliki 62% ya hisa katika mradi huo, Uganda kupitia UNOC ina 15%, Tanzania kupitia TPDC 15% na Kampuni ya China CNOOC ina 8%.  

Catherine ameongeza “Kwa kupita tu mradi huu Watanzania wengi wamenufaika, ni pamoja na wakandarasi wetu wakubwa kwa wadogo wamepata tenda nyingi mbalimbali,” amesema na kuongeza,

“Si tu wakandarasi bali hadi Watanzania wadogo wadogo kwa sababu ajira zetu zinaanzia tangu kwenye ngazi ya kijiji, hivyo tunaajiri katika vijiji vyote ambapo bomba hili limekatiza,” amesema.









Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement