Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Idadi ya watoto 5,410,576 walio chini ya umri wa miaka mitano sawa na 38.8% walipata magonjwa ya maambukizi katika mfumo wa hewa wa juu kwa mfano mafua na kikohozi katika mwaka 2023.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema hayo leo alipotoa taarifa kwa Umma kuhusu hali ya kwa mwaka 2023 na kutaja vipaumbele vya Wizara hiyo kwa mwaka 2024.

Ametaja magonjwa mengine yaliyotesa kundi hilo ni malaria ambapo waliougua walikuwa 1,483,846 [10.7%], kuharisha bila upungufu wa maji watoto 1,68,763 [8.4%].

“Maambukizi katika njia ya mkojo [UTI] watoto 1,050,723 [7.5%], Homa ya Mapafu [Nimonia] 1,029,548 [7.4%].

“Maambukizi ya Ngozi [yasiyo fangasi] watoto 526,983 [3.8%], magonjwa mengineyo ya mfumo wa chakula yasiyo ya kuambukiza 524,698 [3.8%].

Ametaja magonjwa mengine ni ya minyoo watoto 402,425 [2.9%], kuharisha na upungufu wa maji 319,686 [2.3%] na maambukizi ya ngozi [fangasi] watoto 308,353 [2.2%].

Kwa upande wa watu wenye umri wa miaka mitano na zaidi magonjwa 10 yaliyowatesa zaidi Watanzania ni maambukizi katika mfumo wa hewa wa juu wagonjwa 4,901,844 [18.9%].

“Maambukizi katika njia ya mkojo [UTI] 4,095,104 [15.8%], malaria 1,772,523 [6.9%], shinikizo la damu 1,455,165 [5.7%].

“Vidonda vya tumbo 963,520 [3.7%], magonjwa mengineyo yasiyo ya kuambukiza 830,059 [3.2%], homa ya mapafu [Nimonia] 703,666 [2.7%], kisukari 652,455 [2.5%].

Ametaja magonjwa mengine ni ya minyoo 611,538 [2.4%] na magonjwa mchanganyiko 552,661 [2.1%].

Tumeona ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama shinikizo la damu kutoka 2.7% hadi 5.6% kwa mwaka 2023,” amesema na kusisitiza,

“Ugonjwa wa kisukari idadi imeongezeka kutoka 1.6% hadi 2.5%. Amewahimiza Watanzania kuzingatia mtindo bora wa maisha hususan ulaji unaofaa ili kuepuka magonjwa yasiyo ambukiza.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement