Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

‘Darasa’ la mtindo bora wa maisha hususan kuzingatia ulaji unaofaa linalotolewa mara kwa mara kwa jamii na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili [MNH], ni zuri.

Siku za hivi karibuni mafundisho yake yamejizolea umaarufu mkubwa na kuibua mijadala mingi katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Prof. Janabi amekuwa akihimiza wanajamii kuepuka ulaji usiofaa ikiwamo vyakula vya wanga kwa wingi, matumizi ya sukari nyingi na chumvi ya mezani ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza leo na waandishi wa habari kuhusu hali ya utoaji huduma za afya kwa mwaka 2023, amesema jamii haipaswi kupuuza mafundisho ya Prof. Janabi.

“Mafundisho yake hata mimi yananitisha lakini jamii isiyapuuze,” amedokeza na kuongeza,

"Watu wanafanya mzaha na Prof. Janabi na mafundisho anayotoa, japo wakati mwingine hata mimi ananitisha.

“Lakini mimi ni mwanafunzi wake na ‘ameniharibu’ [amenibadilisha] tangu Mei 2023 sinywi chai yenye sukari,” amebainisha Waziri Ummy.

Prof. Janabi kabla ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa MNH amewahi kuiongoza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete [JKCI] kwa takriban miaka saba, uhimiza jamii kuepuka pia unywaji wa pombe.

Amekuwa akieleza madhara makubwa yatokanayo na mtindo mbovu wa maisha, ulaji usiofaa na unywaji wa pombe unavyochangia magonjwa yasiyoambukiza.

Magonjwa hayo katika ripoti yake, Waziri Ummy amesema ni kati ya magonjwa 10 yaliyoongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa Tanzania, mwaka 2023 kundi la wenye miaka mitano na zaidi.

Amebainisha “Tumeona ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama shinikizo la damu kutoka 2.7% hadi 5.6% kwa mwaka 2023.

“Ugonjwa wa kisukari idadi imeongezeka kutoka 1.6% hadi 2.5%. Amewahimiza Watanzania kuzingatia mtindo bora wa maisha hususan ulaji unaofaa ili kuepuka magonjwa yasiyo ambukiza.

Pamoja na hayo, magonjwa ya maambukizi katika mfumo wa hewa wa juu imerekodiwa idadi ya wagonjwa 4,901,844 [18.9%].

“Maambukizi katika njia ya mkojo [UTI] 4,095,104 [15.8%], malaria 1,772,523 [6.9%], shinikizo la damu 1,455,165 [5.7%].

“Vidonda vya tumbo 963,520 [3.7%], magonjwa mengineyo yasiyo ya kuambukiza 830,059 [3.2%], homa ya mapafu [Nimonia] 703,666 [2.7%], kisukari 652,455 [2.5%].

Ametaja magonjwa mengine ni ya minyoo 611,538 [2.4%] na magonjwa mchanganyiko 552,661 [2.1%].

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement