Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Siku 69 za mapambano ya kudhibiti ugonjwa wa virusi vya Marburg ndani ya Mkoa wa Kagera, zimeiandikia historia ya kipekee Tanzania, ulimwenguni.

Tanzania ni nchi iliyoweza kukomesha ugonjwa huo kwa kipindi kifupi zaidi kuliko nchi nyingine ambazo zimewahi kupata mlipuko.

Yameelezwa hayo leo Dar es Salaam na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alipowasilisha taarifa ya hali ya utoaji huduma za afya Tanzania kwa mwaka 2023 kwa waandishi wa habari.

Kwa mwaka 2023, nchi yetu iliweza kupambana na kudhibiti ugonjwa wa Marburg Mkoa wa Kagera ambapo jumla ya Visa 9 na Vifo 6 vilitolewa taarifa,” amesema.

Ameongeza “Wizara kwa kushirikiana na wizara nyingine pamoja na wadau wengine wa Afya ilifanikiwa kudhibiti mlipuko ndani ya siku 69.

“Tofauti na nchi nyingine ambazo huchukua hadi miezi 6 kudhibiti milipuko kama hii.

Amesema katika kipindi hicho Wizara imeendelea kufuatilia mwenendo wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa.

“Maambukizi ya UVIKO 19  yaliongezeka nchini kutoka wastani wa visa 12 bila kifo kwa wiki  kwa Mwezi Julai 2023 hadi wastani wa visa 21 bila kifo kwa wiki kwa mwezi Desemba, 2023.

Amesema Maambukizi ya Influenza yalikuwa 903 bila kifo kwa mwaka 2023, tulipata ugonjwa wa Kimeta mikoa ya Kilimanjaro, Songwe, Arusha na Rukwa.

“Idadi ya wagonjwa wa Kimeta walikuwa 76 na kifo 1,” amesema Waziri Ummy.

Amesema kwa upande wa ugonjwa wa kipindupindu Wizara ilitoa ripoti ya mikoa 12 ambapo wagonjwa 927 na vifo 27 vilitolewa taarifa.

Mkoa wa Arusha uliongoza kwa visa 214 lakini bahati nzuri hakukutokea kifo, katika mkoa wa  Mara jumla ya visa 193 na vifo vinane vilitolewa taarifa.

“Mkoa wa Simiyu Visa 184 na vifo viwili, mpaka sasa kuna mikoa 6 ambayo inaendelea na mlipuko, ambayo ni Shinyanga, Rvuma, Tabora, Simiyu, Mwanza na Kagera,” ameitaja.

Amesema Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu atatoa taarifa ya kina siku si nyingi juu ya mwenendo wa ugonjwa huo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement