Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Idadi ya wagonjwa kutoka nje ya nchi wanaofuata huduma za matibabu nchini Tanzania imezidi kuongezeka kutoka 5,705 mwaka 2022 hadi 6,931 mwaka 2023.

Ongezeko hilo ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali wa uboreshaji huduma za kibingwa na bobezi.

Wagonjwa hawa wanatoka nchi za Comoro, Malawi, Burundi, Zambia, Congo DRC, Uganda, Zimbabwe na Kenya,” amebainisha Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy alikuwa akitoa taarifa ya Hali ya Utoaji Huduma kwa mwaka 2023 katika mkutano wake na waandishi wa habari, mapema leo Dar es Salaam.

Ameongeza “Wagonjwa hawa walihudumiwa katika hospitali 6 ikiwamo Hospitali ya Taifa Muhimbili [MNH], Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

Amebainisha hospitali nyingine ni Taasisi ya Mifupa MOI Aga Khan na Safee ambazo zenyewe ni za sekta binafsi.

“Tanzania imekuwa kimbilio la wagonjwa kutoka nje ya nchi, na wagonjwa hawa wanaleta fedha za kigeni na hivyo kuchangia pato la Taifa,” amesema.

Amesisitiza kwa upekee wa Kiuchumi na kijiografia wa Tanzania ikiwamo uanachama hai wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC, kuzungukwa na nchi nane na kuwa na  Bahari ya Hindi,

.., kama mpaka wake upande wote wa mashariki, kumeifanya kuwa  “Lango la Afrika”.

“Kunatuweka kwenye fursa adimu ya kuwa “Kitovu cha Tiba Utalii” katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini,” amesisitiza Waziri Ummy.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement