Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Picha kwa hisani ya mtandao.

Na Veronica Mrema

Kila mwaka kuna wanawake wapatao milioni 2 ambao hubeba ujauzito, jamii imeonekana kuwa na mwamko mzuri wa kuzingatia mahudhurio manne ya kliniki, Tanzania.

Eneo la huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ni kati ya yaliyofanyiwa tathmini na Wizara ya Afya kwa mwaka 2023 kwa kuzingatia viashiria vikuu 16.

Miongoni mwa viashiria hivyo ni mahudhurio angalau mara nne au zaidi [ANC Visit] kwa kundi hilo.

Moja ya kiashiria kikuu cha ubora wa huduma za afya nchi yoyote duniani ni kuwa na kiwango cha wajawazito wanaojifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Ripoti ya Wizara ya Afya ya Hali ya Utoaji Huduma kwa mwaka 2023 imeeleza kwa mwaka 2023 wajawazito 2,391,427 [97.5% walihudhuria Klinic mara nne katika kipindi cha ujauzito wao.

Hata hivyo idadi hiyo imetajwa kushuka kidogo kulinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2022.

Ripoti hiyo imeeleza katika mwaka huo wajawazito 2,442,580 [102%] walihudhuria kliniki mara nne katika kipindi cha ujauzito wao.

Licha ya hali kuwa hivyo, bado Tanzania ipo katika lengo iliyojiwekea kufikia 80% mwaka 2030 kama ambavyo pia imeelekezwa na Shirika la Afya Duniani [WHO].

“Hii inaonesha, Watanzania wana mwamko mkubwa na wanatambua umuhimu wa wajawazito kufanya mahudhuria ya kliniki wakati wa ujauzito ili kupata huduma stahiki,”.

Ni kauli yake Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ambapo pia amesisitiza “Hili ni eneo ambalo nalipenda na ndipo ulipo ‘moyo’ wa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Tumepita lengo lililowekwa na WHO pamoja na Mpango [wetu] Mkakati wa Kuimarisha Huduma za Afya ya Mama na Mtoto [One Plan III],” amesema.

Ameongeza “Mahudhurio ya kliniki yanaonesha wajawazito wana imani na huduma zinazotolewa na wanatambua umuhimu wa kuhudhuria kliniki wakati wa ujauzito ili kupata huduma sahihi.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement