Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Na Veronica Mrema

Utoro ni zao la uhalifu, baadhi ya watoto waliopo shuleni hujificha kwenye makorongo na maeneo mengine mbalimbali ambako huko hutekwa na vijana wakubwa na kufanyiwa uhalifu.

Ikiwamo kuvutishwa bangi, kubebeshwa au wao kulawitiwa hali hiyo imeifanya Jeshi la Polisi kuja na mbinu ya kusaidia kuokoa kizazi cha Tanzania.

‘Pembe tatu’ madhubuti ni nyenzo iliyoundwa, inayotumika kuwaokoa/kuwapuesha watoto dhidi ya janga la matumizi na biashara ya dawa za kulevya,

 Askari A/INSP Verediana Milimba ambaye ni Mkaguzi Msaidizi Wilaya ya Dodoma Mjini [Kitengo cha Ushirikishwaji Jamii - Polisi Kata- Kata ya Hazina] anafafanua zaidi,

“Tumeweka mikakati mbalimbali ambayo kwa kiwango kikubwa inatusaidia kuifikia jamii," Askari A/INSP Verediana Milimba anafafanua.

Ni Mkaguzi Msaidizi Wilaya ya Dodoma Mjini [Kitengo cha Ushirikishwaji Jamii - Polisi Kata- Kata ya Hazina] anasema wanshirikia na DCEA [Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya].

“Sisi tumeweka mikakati ambayo kwa kiasi kikubwa inatusaidia kufikia jamii kwa ujumla," anasema.

anabainisha Mkakati wa kwanza ni mradi wa usalama wetu kwanza ambao umelenga zaidi watoto walioko ma-shuleni kuanzia shule kuanzia ya msingi, sekondari na vyuo.

“Lengo kuu kwanza ni kudhibiti utoto kwa sababu tumegundua ni zao la uhalifu wanajificha kwenye makorongo, maeneo mbalimbali wanatekwa na vijana wakubwa kufanyiwa uhalifu.

“Ikiwamo kuvutishwa bangi, kubebeshwa ama wao kulawitiwa,” anasema na kusisitiza,

“Kwa hiyo tulianza kwanza kukemea [utoro], tulitengeneza ‘pembe-tatu’ kuanzia Polisi [askari], walimu, DCEA na mzazi ili kudhibiti utoro.

“Halafu tunawapa elimu wao kukataa kuwa wasambazaji kwa namna yoyote ile, kwa maana abebe mzigo kama mtu amempatia ajue amebeba nini.

“.., na asipojua leo kabeba nini, kupeleka wapi, basi atoe taarifa kwa mwalimu rafiki kwa maana ya program rafiki za msingi au sekondari.

Anafafanua “.., kwamba leo nimebeba kitu fulani, kupeleka sehemu fulani na sikijui, ili tuweze kufanya ufuatiliaji alibeba nini na zaidi tunawaambia hata kwa kutokujua watoe taarifa.

Anasema wanashirikiana kwa ukaribu na DCEA katika kutambua wajasiriamali wote wanaofanya biashara katika maeneo ya shule.

“Shule zetu zimezungukwa na wajasiriamali wengi ambazo hazina uzio, kwa hiyo unakuta kuna muingiliano mkubwa kati ya watoto na raia.

“Tunachokifanya ni kuhakikisha tunawatambua wajasiriamali wote ambao wapo ndani ya maeneo ya shule tunafanya nao vikao na kuwapa elimu.

Anasisitiza “.., na tumetoa ombi rasmi kwa wakuu wote wa shule kuwaomba wawatambue kwa vitambulisho ili kuepusha wale wanaopita kwa njia kwamba wamepita ameuza akaondoka.

“Isije ikatokea wale wenye nia ovu kuzalisha waraibu wapya katika rika la watoto, licha ya hivyo tunawapa watoto pia elimu wajitahidi kununua vitu ambavyo viopo ndani ya mipaka ya shule.

“Ambayo sisi tumejiridhisha hawa wajasiriamali sisi tumeshawahihi na tumejiridhisha hawa tumeshawahihi na tunafanya ufuatiliaji hata historia zao za nyuma,” anasema.

Anasema wanahamasisha watoto wasivuke nje ya shule kwenda ng’ambo ya barabara ambapo si sehemu ya wale wajasiriamali waliotambuliwa.

Anasema wanahimizwa siende kufuata bidhaa ili kuwaepusha kuwa waraibu kupitia zile bidhaa ambazo zinauzwa.

Juhudi za kuokoa kizazi cha Tanzania haifanyiki ndani ya shule na vyuo pekee, DCEA imezidi kuongeza nguvu ndani ya jamii kupambana na ‘mapapa wa unga’.

Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo anasema jamii imeendelea kupewa elimu kuhusu Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya namba 5 ya mwaka 2015.

Anasema Sheria hiyo inatoa adhabu kali kwa makosa mbalimbali yanayohusiana na makosa ya dawa za kulevya.

“Ukikamatwa unajihusisha, unasafirisha, unauza, unatumia. Sheria yetu inaweza kukufunga hadi kifungo cha maisha gerezani,” anasema.

Anaongeza “Ndiyo maana tupo katika wiki ya sheria kwa sababu mahakama ni mdau wetu mkubwa katika mnyororo wa haki jinai.

“Tunashirikiana na mahakama na taasisi zote za haki jinai kutoa elimu kwa wananchi ili wajiepushe na biashara ya dawa za kulevya.

Anasema katika oparesheni mbalimbali wanazozifanya tumebaini watoto wengi hasa wale wanaoacha shule, wanaotelekezwa mitaani ndiyo wengi wanaotumika.

“…, katika usafirishaji wa dawa za kulevya katika maeneo mbalimbali,” anasema na kuongeza,

“Watu wanatumia nafasi hizo kwa wale watoto katika kuwatumia kumeza dawa za kulevya na kusafirisha maeneo mbalimbaliu.

“Wengine wanawatumia kusafirisha maeneo mbalimbali kutokana na kwamba wakiamini wale watoto hawawezi wakagundulika mapema.

Anasema baada ya kubaini hilo sasa DCEA inashirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanatoa elimu vijijini, mijini [mitaani], familia kwa familia kuhimiza wazazi kulea vema watoto wao.

“Wazazi watambue tabia za watoto wao mapema ili wasishiriki katika tabia hiyo [isiyofaa] ili pia wahakikishe wanalinda watoto wao .

“.., wasije wakatumika katika kusafirisha dawa za kulevya kwa sababu katika kushiriki kumeza wakati mwingine ukimeza lazima uonje kidogo dawa za kulevya.

“Ili uweze kumudu kubeba kwa muda mrefu, mwisho wake unajikuta yule mtoto anayetumika katika kubeba dawa za kulevya naye anakuwa mtumiaji, mraibu wa dawa za kulevya.

Anaongeza “Unakuta tatizo la dawa za kulevya linaendelea, tutoe rai wazazi, viongozi wa dini, familia na jamii kwa ujumla tushirikiane watoto wasiingie katika matumizi ya dawa za kulevya.

ORODHA YA 'RIMOTI'

Anasema DCEA inaendelea kubaini mitandao ya ‘mapapa wa unga’ wanaojihusisha na biashara haramu ya cocaine, heroin na metamphetamine.

Kamishna Jenerali Lyimo anasema wanaendelea kubaini pia hadi mtandao wa wakulima wakubwa wa dawa za kulevya za mashambani ikiwamo bangi na mirungi.

“Orodha tuliyonayo sasa hivi tumebaini wengi wanafanya biashara hii kwa ‘rimoti’ [yaani] wapo lakini hawafanyi [waziwazi].

“Wanawatumia watu, tumeshawatambua [‘mapapa’ hao] tunayo orodha na wale wanaofanya [kwa ‘rimoti’] tunayo.

Anasisitiza “Tutawaunganisha na tunajua na wengine wana biashara zao kubwa tu [zisizo za ‘unga’/wamejificha humo].

“Tuwaonye waache hiyo biashara tutawakamata na mwisho wa siku watadhalilika, waache biashara hiyo [ya ‘unga’].

“.., watafute biashara halali za kufanya ili tujenge Taifa letu, uchumi wetu na ustawi wa jamii tuhakikishe biashara ya dawa za kulevya inaisha,” anaesisitiza.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement