Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Utekelezaji mzuri wa kitita cha PEN-Plus kwa wenye Magonjwa Yasiyoambukiza [NCD’s], Halmashauri ya Kondoa na Halmashauri ya Katavi, umeipa heshima kubwa Tanzania Barani Afrika.

Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutekeleza vema PEN-Plus hatua ambayo imeipa fursa ya kuzipa somo nchi nyingine Barani humo ili kuongeza nguvu ya mapambano dhidi ya NCD’s.

Ni kwa mantiki hiyo imekuwa mwenyeji wa Mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kujadili Namna ya Kukabiliana na NCD’s Barani Afrika ili kufikia Malengo Endelevu ya Duniani [SDG’s].

“Jambo zuri wote [Afrika] tuna nia moja ya kupambana na NCD’s, tumeona mtoto wa Tanzania [mgonjwa wa NCD’s aliyefikiwa na PEN-Plus] kwa muda mrefu alishindwa kwenda shuleni.

“Lakini sasa ameweza kurudi shuleni,” amesema Mkuu wa Idara ya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa AfricaCDC Dkt. Mohammed Abdulaziz.

Dkt. Abdulaziz alikuwa akizungumza wakati wa hafla ya ufungaji wa Mkutano wa   Kujadili Namna ya Kukabiliana na Magonjwa Yasiyoambukiza Barani Afrika [ICPPA].

Mkutano huo wa kwanza wa Kimataifa ulioratibiwa na Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika [AFRO-WHO] umefanyika April 23 hadi 25, 2024 Dar es Salaam, Tanzania.

“Ni lazima tuweke mikakati bora ili kutatua changamoto za ki-afya katika eneo la NCD’s, lazima tuwaangalie hawa wagonjwa wanahitaji huduma sawia, uhakika wa matibabu na upatikanaji dawa.

Amesisitiza Dkt. Abdulaziz kwamba ni muhimu mapambano dhidi ya NCD’s yakahusisha jamii moja kwa moja kwa kuipa elimu sahihi ili kuondosha unyanyapaa kwa wale wanaougua.

“Tunahitaji kuendelea kuangazia haya na AfricaCDC tupo tayari kuunga mkono ili kufikia lengo na kupata matokeo chanya,” amesema.

PEN-Plus ni kitita maalum cha huduma muhimu anazopewa mtu mwenye ugonjwa usioambukiza katika vituo vya afya vya msingi [Primary Health Facilities].

“Kwa pamoja Afrika tuna mkakati wetu na tulikutana kuweka mikakati yetu kwamba tunakwenda ili kuweza kupambana na NCD’s,”.

Ni kauli yake Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Tanzania Dkt. Hemed Nyenbea alipomwakilisha Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katika kufunga mkutano huo.

Ameongeza, “Lakini pia tulikuwa tukitekeleza [mkakati] kuendana na malengo ya dunia [Endelevu – SDG’s].

“.., ambayo yaliwekwa ili kupunguza vifo vitokanavyo na NCD’s angalau kufikia 25% ifikapo 2030,” amebainisha.

Amesisitiza ni mkutano wa kwanza wa aina yake kufanyika Afrika ukiwa na agenda ya kupambana na NCD’s

“[Kimsingi] mapambano dhidi ya NCD’s yameanza muda mrefu kidogo Afrika.., ila ni namna gani tuje pamoja kuweza kuweka mikakati, wamekuja Tanzania.

“Tanzania imekuwa ndiyo nchi ya kwanza kuanza kutekeleza vema mkakati huu,” amebainisha.

Ameongeza “Tulianza na PEN ilikuwa kitita cha huduma muhimu kwa wenye NCD’s katika ngazi ya msingi [Halmashauri hadi zahanati] tulifanya vizuri kwa kaisi kikubwa.

“Ilionekana haitoshi kuna watu wanaumwa sana mpaka wanapata changamoto nyingi na kuhitaji rufaa kwenda hospitali kubwa.

“Ikaonekana kuna haja ya kupeleka hizi huduma mpaka kule chini kabisa wlaipo wananchi ndiyo tunaita PEN-Plus.

Amesisitiza “Tumetekeleza Halmashauri mbili Kondoa na Karatu mpaka wengine [kutoka nchi nyingine za Afrika] wamekuja kujifunza.

“WHO ikaona Tanzania ni nchi sahihi kabisa kufanya kongamano la kwanza, ndiyo maana tumelileta hapa wamefurahia, wamejifunza wamekuja hadi kutuuliza.

“Mpaka namna takwimu zetu zinavyopatikana tumewaeleza, lengo la Serikali ni kuhakikisha mkakati huu unakwenda nchi nzima,

Amebainisha “Kama tunavyojua wananchi wengi wanapata huduma ngazi za msingi, 80% wanaenda huko kwa sababu ndiyo za kwao na wanaenda kule na wagonjwa wengi wapo kule.

“Ili kuweka usawa na kupunguza gharama kwa wananchi lengo ni kupeleka hizi huduma ngazi za msingi, halmashauri zote, vituo vya afya na hospitali ambako ndiko kuna wananchi wengi,”.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement