Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Ni ‘askari’ waliojaliwa kupata maarifa lukuki ambayo kwa kiwango kikubwa yanahitajika ndani ya jamii kwa usahihi wake na kwa wakati ili kuijenga vema afya ya akili na ustawi imara kwa manufaa ya Taifa.

Madaktari wanao uwezo wa kuisaidia jamii kwa kuipatia elimu sahihi hatimaye ikapata matokeo chanya na bora kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake, Watoto na Makundi Maalum imefungua milango yake wazi kwa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania [MEWATA] ili ishiriki bega kwa bega kuiokoa jamii.

Waziri Dkt. Dorothy Gwajima katika Mkutano Mkuu wa 21 wa MEWATA Dar es Salaam amesema MEWATA ina nguvu kubwa na nafasi nzuri ya kuielimisha jamii ili kutokomeza vitendo vya ukatili.

“Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunda wizara hii maana yake ni kwa ajili ya sekta zote zinazoratibu mambo ya maendeleo ya jamii,” amesema.

Ameongeza “Mambo mengi tunayaona huku juu kama changamoto watu wanauana, wanaharibiana, ukatili wa ki-jinsia [ndani ya jamii].

“Ndoa zinavunjika [kuna] migogoro, mifarakano, tunaona watoto wa mitaani, mila kandamizi, desturi kandamizi,” amesema.

Amebainisha “Tunaona maamuzi ya jamii yatokanayo na imani hasi, MEWATA itaenda kwenye jamii kutoa elimu.

“.., ya jinsi gani maamuzi hayo wanayoyafanya na taratibu wanazofanya baadae ndiyo tunakutana na ‘presha’ [Shinikizo la Damu] huko na magonjwa mengine sugu.

“UKIMWI, Kisukari, Ulemavu [na] Msongo wa mawazo unaosababisha athari sasa [hivi] za maisha.

“Watu wanajikatili [na] wanakatili wengine, wanaishi na ustawi mdogo wa ki-afya,” amesema.

Waziri Gwajima amesema ikiwa MEWATA watakwenda kule chini [ngazi ya jamii] wataweza kuelimisha na hatimaye kutokomeza utaratibu huo mbovu wa maisha unaozalisha matatizo mengi.

“MEWATA wana nafasi kubwa sana, kwa sababu hata Vitabu Vitakatifu [vya kiimani/kidini] vinasema watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa.

“Lakini wanatakiwa wamshike sana elimu asiende zake ili waweze kupona na kupata baraka sasa nani wa kupeleka [elimu] kwenye jamii?.

“.., hayo maarifa MEWATA kama wanawake madaktari wana nafasi kubwa,” amesema na kuongeza,

“Tumewakaribisha waje ofisini kwetu, tuingie nao mkataba tuweke mkakati, kufika kwenye jamii tukifanya hivyo, tutaifungua jamii yetu wakaelewa kwamba kumbe ustawi wa afya zao.

Amesisitiza “Ustawi na utulivu hata katika vipato vyao, watatulia. Ila uchumi unateketea hawafanyi maamuzi mazuri.

“Kwamba tutunze, tule vizuri hata hizi tupate huduma nzuri za afya kwa sababu vituo vimejengwa na Serikali.

“Ni kwa sababu ya mfumo finyu wa fikra, na kukosa elimu ambayo MEWATA wakiipeleka tutayapunguza mengi ... Wizara hii tunawakaribisha,” amesema.

Rais wa MEWATA Dkt. Zaitun Bokhary amemshukuru Waziri Dkt. Gwajima kwa kuwafungulia mlango na kwamba nafasi hiyo wataitumia vema kwa ajili ya kuisaidia jamii.

“Huu ni mkutano wetu mkuu wa Chama [ambao hufanyika] kila mwaka [mwaka huu] kauli mbiu yetu ni ‘Pioneering Women Health’.

“Kwa kuwa tunaingazia afya ya mwanamke, tuliona yeye ndiye Waziri mwenye dhamana ya wanawake, watoto na makundi maalum aje atupe mada inayohusiana na afya ya mwanamke.

Dkt. Zaituni ambaye pia ni Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili [MNH] ameongeza,

“[Pamoja] na changamoto ambazo anapata kwenye wizara yake.Tunashukuru amefungua mlango kwetu MEWATA twende ofisini kwake.

“.., kushirikiana kuongelea afya ya mwanamke bila aibu kwa uwazi kabisa. Kwa sababu inaonekana kuna changamoto nyingi wanapata wanawake ila hazizungumzi.

“Ametufumbua macho [na] ametufungulia malango hatutailazima damu [hii nafasi] tutakwenda ofisini kwake kuangalia namna tutakavyotangaza hiyo eilimu na hususan maeneo ya vijijini,” amesema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement