Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Chanjo ya HPV ina uwezo wa kukinga dhidi ya kirusi cha HPV ambacho husababisha saratani ya mlango/shingo ya kizazi lakini haihusiani kabisa na masuala ya uzazi wa mpango.

Jamii imehimizwa kuondoa hofu, woga na wasiwasi juu ya chanjo hiyo kwani shahidi za ki-sayansi zimethibitisha ni salama na ina ufanisi katika kumkinga msichana.

Rai hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alipofungua Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Kukweka Mipango na Mikakati ya Kupambana na Magonjwa Yasiyoambukiza Afrika.

Mkutano huo [ICPPA] umeandaliwa na Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika [AFRO-WHO] umehudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 kutoka mataifa mbalimbali Barani humo.

“Tunaweza kutokomeza saratani ya mlango wa kizazi kama tutawapa watoto chanjo ya HPV,” amesema.

Amesisitiza “[Saratani ya mlango/shingo ya kizazi] tuugue sisi [wanawake] ambao bado hatukupata chanjo [ya HPV].

Chanjo hiyo inatolewa kwa wasichana ambao bado hawajaanza kujamiiana ili kuwakinga dhidi ya kirusi hicho cha HPV ambacho ndicho husababisha saratani hiyo.

Tanzania kupitia Wizara ya Afya imelenga kuwafikia wasichana Mil. 4,841,298 wenye umri wa miaka 9 hadi 14 ifikapo Desemba, 2024.

Sayansi imethibitisha dozi moja ya chanjo ya HPV inatosha kabisa kuupa mwili wa msichana uwezo wa kinga, dhidi ya kirusi hicho mbacho ni tishio kubwa hivi sasa duniani.

Waziri Ummy amesisitiza chanjo hiyo ni salama na kuongeza, “Chanjo inatolewa kwa wasichana ambao hawajaanza kujamiiana.

“Kwa sababu kirusi kinatoka kwa mwanaume kuja kwa mwanamke. Tunaamini watoto wa miaka 9 hadi 14 hawajaanza kujamiiana.

“Tunategemea miaka 15 -20 kizazi kilichokuwa na miaka 14 kwenda mbele kisiwe na saratani kabisa Tanzania hilo jambo linawezekana,” amesisitiza.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement